Showing posts with label KIMATAIFA. Show all posts
Showing posts with label KIMATAIFA. Show all posts

WAZIRI APIGWA KOFI UFARANSA

06:30 Add Comment

Waziri mkuu mstaafu wa Ufaransa Manuel Valls amekashifiwa alipokuwa akihamasisha katika kampeni za chama cha kisoshalisti katika uchaguzi mkuu wa kiti cha Urais nchini Ufaransa.
Alipokuwa akihutubia katika ukanda wa Magharibi mwa mji wa Brittany alipigwa kofi na kijana mdogo alipokuwa akisalimia kwa kushikana mikono.
Mlinzi binafsi wa Bwana Valls alimkamata kijana huyo kooni kisha akamtupa chini.
Manuel Valls hajajeruhiwa katika tukio hili.

WAFUNGWA 30 WAFARIKI KATIKA MACHAFUKO BRAZIL

06:14 Add Comment

Taarifa za kutisha zimeanza kujitokeza nchini Brazil kutokana na machafuko yaliyotokea usiku kucha katika jela la Alcaçuz baada ya kuibuka kwa mgomo.
Mamlaka nchini Brazil zinasema takriban wafungwa thelathini waliuawa na wafungwa wenzao, wataalamu wakuchunguza masuala ya mauwaji wamesema walioathirika zaidi walikuwa wamekatwakatwa au kutolewa baadhi ya viongo.
Mgomo huo ulianza jumamosi mchana, wanakikundi wa kikundi cha wahalifu waliopo katika magereza ya Brazil na kushambulia kundi hasimu lenye msimamo tofauti.
Hii ni mara ya tatu kwa mgomo mkubwa kama huu kujitokeza kwa wafungwa nchini Brazil mwezi huu, mamia ya wafungwa wamefariki gerezani katika miji ya Amazonas na Roraima.

UTAMBUE MJI WA KWANZA KUUKARIBISHA MWAKA MPYA

16:46 Add Comment

Mji wa Auckland nchini New Zealnd ndio mji wa kwanza duniani kuukaribisha mwaka mpya wa 2017.
Fataki zilirushwa kutoka jengo refu katikati mwa mji huo.
Polynesia na visiwa vya Pacific ikiwemo Samoa, Tonga na kiribati pia viliukaribisha mwaka mpya.
Miji mingi duniani imeimarisha usalama kwa sherehe za mkesha wa mwaka mpya baada ya mwaka ambapo washambuliaji waliendesha malori katika umati wa watu mjini Berlin na Nice.
Mjini Paris Madrid na New York vizuizi vya simiti na magari yaliobeba mizigo mizito yatatumiwa kuzuiwa bustani zilizopo mjini ambapo watu wengi hukongamana ili kusherehekea.

KIJANA ALIEPANGA KUMUUA TRUMP AFUNGWA

06:18 Add Comment

Mwanamme mmoja raia wa Uingereza amehukumiwa kifungo cha miezi 12 jela kufuatia jaribio lake la kutaka kunyakua bunduki kwa lengo la kumuua Donald Trump.
Michael Sandfgord mwenye umri wa miaka 20 alikiri makosa hayo ya kumiliki bunduki na kuvurua mkutano.
Analaumiwa kwa kujaribu kunyakua bunduki kutoka kwa polisis wakati wa mkutano wa hadhara huko Las Vegas ili kumfyatulia risasi mgombea urais.

Mahakama ilisema kuwa huenda akaachiliwa baada ya miezi minne ambapo atasafirishwa hadi nchini Uingereza
Baada ya Sandford kukamatwa aliwaambia maafisa kuwa alikuwa na mpango wa kumpiga risasi Donald Trump.
Hata hivyo hakufanikiwa kunyakua bunduki kutoka kwa afisa wa polisi.
Mamake alisema kuwa alikuwa amepoteza mawasiliano na mwanawe, ambaye aliondoka nyumbani kutembea kote marekani mwaka 2015.
Kulingana na nyaraka za mahakama Sandfords ambaye hakuwa na makao na ambaye alikuwa akiishi Marakani kinyume na sheria baada ya muda wa visa yake kuisha, aliiwaambia majasusi kuwa aliendesha gari kutoka California hadi Nevada kwa lengo la kumpiga risasi Trump.
Anaripotiwa kumuambi afisa wa polisi kuwa alitarajia kuuawa kwenye shambulizi hilo na kwamba alikuwa na tikiti za kuhudhuria mkutano mwingine wa Trump baadaye ikiwa angapata fursa ya pili.
Majaji walitaja kitendo hicho kuwa cha kustaajabisha.

AGUERO OUT MECHI NNE

23:34 Add Comment

Mshambuliaji wa Manchester City Sergio Aguero amepigwa marufuku kucheza mechi nne baada yake kufukuzwa uwanjani kwa uchezaji mbaya mara ya pili msimu huu.
Aguero, 28, alifukuzwa uwanjani kwa kumchezea visivyo beki wa Chelsea David Luiz wakati wa mechi ambayo City walilazwa 3-1 nyumbani Ligi ya Premia siku ya Jumamosi.
Mshambuliaji huyo wa Argentina alikuwa ameadhibiwa tena mwezi Agosti alipopewa kadi nyekundu kwa kumchezea visivyo mchezaji wa West Ham Winston Reid.
Atakosa mechi za City dhidi ya Leicester, Watford, Arsenal na Hull.

Mwenzake wa City Fernandinho pia alifukuzwa uwanjani alipokabiliana na Cesc Fabregas baada ya madhambi hayo ya Aguero na amepigwa marufuku kucheza mechi tatu.

MITANDAO KUDHIBITIWA

23:31 Add Comment

Kampuni kubwa za kiteknolojia Duniani zimeanzisha programu mpya itakayosaidia kupunguza kasi ya uchochezi na misimamo mikali mitandaoni.
Twitter, Facebook, na Microsoft watakapo baini kuwepo kwa taarifa za aina hiyo wata zitambulisha kwa alama maalumu.
Suala hili litahimiza umakini ili kurahisisha utambuzi wa taarifa chochezi zitatokea katika mitandao yao.
Kampuni hizo zimearifu kuwa mchakato huo hauta jiendesha wenyewe ili kuepusha upotoshaji usiotarajiwa kwa waandishi na taarifa nyingine zinazo ashiria vurugu japo kuwa hazi chochei moja kwa moja