MAKAMU Mwenyekiti wa CCM, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein, leo anatarajia kukiongoza Kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa mjini hapa.
Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Katibu wa Kamati Maalumu ya NEC Zanzibar - Idara ya Itikadi na Uenezi, Waride Bakar Jabu, kikao hicho cha kawaida cha siku moja kitafanyika Ofisi Kuu ya CCM, Kisiwandui kuanzia saa 4 asubuhi.
Alisema kikao pamoja na mambo mengine, kitapokea na kujadili Mapendekezo ya wanachama wa CCM wanaoomba kuteuliwa kugombea nafasi ya Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Dimani na kuongeza kuwa maandalizi yote yamekamilika.
Aidha, Katibu Waride alisema kikao hicho kilitanguliwa na Kikao cha Sekretarieti ya Kamati Maalum ya NEC, chini ya Mwenyekiti wake Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai, kwa lengo la kuandaa ajenda za kikao hicho.
Wanachama wa CCM watatu wamepitishwa kuingia katika tatu bora katika kikao cha halmashauri ya jimbo la Dimani ambao ni Juma Ali Juma, Hussein Migoda pamoja na Abdalla Sheria ambao wataajaza nafasi ya mbunge wa jimbo hilo Hafidh Ali Tahir, aliyefariki dunia b aada ya kuugua ghafla usiku wa kuamkia Desemba 11 akiwa katika vikao vya Bunge mjini Dodoma.
Next
« Prev Post
« Prev Post
Previous
Next Post »
Next Post »
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
EmoticonEmoticon