AL SHABAB WAMESHAMBULIA MJI WA AFGOYE

21:19

Wapiganaji wa kundi la al-Shabab nchini Somalia wameushambulia mji muhimu wa Afgoye,yapata kilomita 30 kutoka mji mkuu wa Mogadishu.
Kuna ripoti kuhusu mlipuko wa bomu lililotegwa ndani ya gari na mapigano makali,hususan karibu na afisi za serikali na kituo cha polisi.
Wakazi wameiambia BBC kwamba raia wengi pamoja na wanajeshi wamejeruhiwa.
Al-Shabab limesema kuwa wapiganaji wake wameuteka mji huo,lakini gavana wa jimbo hilo amesema kuwa wanajeshi wa serikali ya Somalia bado wanawakabili wapiganaji hao.
Mji wa Afgoye uko mkabala na barabara kuu inayounganisha Mogadishu na kusini mwa Magaharibi ya Somalia.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »